Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akisikiliza kwa umakini maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Msaidizi Bw. Renatus Mkude juu ya majukumu na huduma mbalimbali zinazotolewa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakati alipotembelea katika banda hilo tarehe 26 Juni, 2025 Jijini Dodoma.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo akiwa na Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kushiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupiga Vita Dawa za Kulevya yaliyofanyika tarehe 26 Juni, 2025 Jijini Dodoma.
Wanachama wa Chama cha Akiba na Mikopo cha Ofisi ya Taifa ya Mashtaka (MASHTAKA SACCOSS) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada kushiriki kwenye Jukwaa ka Maendeleo ya Ushirika Mkoa wa Dodoma lililofanyika katika ukumbi wa Chimwaga.
Watumishi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiwa katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (MeiMosi) ambapo Kitaifa imeadhimishwa tarehe 01 Mei, 2025 kwenye viwanja vya Bombadia Mkoani Singida.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka walioshiriki kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) yaliyofanyika tarehe 1 Mei, 2025 Mkoani Singida
Jaji Mfawidhi wa Mahamaka Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Rose Ebrahim akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo kwa wadau wa Haki Jinai kuhusiana na Uchunguzi wa Makosa ya Kifedha na Uchunguzi wa Kisayansi yaliyofanyika Mkoani Morogoro.
Jaji Mfawidhi wa Mahamaka Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro Mhe. Rose Ebrahim akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa Mafunzo kwa wadau wa Haki Jinai kuhusiana na Uchunguzi wa Makosa ya Kifedha na Uchunguzi wa Kisayansi yaliyofanyika Mkoani Morogoro.
Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka Bi. Bibiana Kileo akikata keki kuashiria upendo na umoja kwa wanawake wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kushiriki kwenye kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani ambayo kitaifa yalifanyika tarehe 8 Machi, 2025 Jijini Arusha.
Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu akisalimiana na Mkuu wa Hifadhi ya Mikumi Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TANAPA, Augustino Masesa mara baada ya kutembelea hifadhi ya Mikumi.
Picha ya pamoja ikijumuisha Mkurugenzi wa Mashtaka Bw. Sylvester Mwakitalu, Mkuu wa Hifadhi ya Mikumi Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi TANAPA, Augustino Masesa wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Ofisi ya Taifa ya Mashtaka mara baada ya kutembelea hifadhi ya Mikumi